.....Kikosi cha Damu chafu
Mkuu wa Wilaya Mhe Kilakala kushoto akimkabidhi mfanowa hundi ya Milion 4 Nahodha wa Damu Chafu Saddy Mapuya
.......Mapuya akiwa na kombe
Rais Ayub akiwa na vijawa wake wakizunguka uwanja wa Saba saba wakati timu yake ikisaka ushindi
.......Rais Ayub wa mbele aiyechutama akiwaongoza vijana wake kuomba dua siku moja kabla ya fainali kwenye maskani ya timu hiyo......Rais Ayub akiwashukuru mashabiki baada ya timu yake kuibuka mabingwa
Rasis Ayubu akizungumza na Mtandao huu juzi
Na Dustan Shekidele. Morogoro.
MTANDAO Mpendwa wa shekidele umeandaa makala Maalum ya Michuano ya Planet Ndondo Cup iliyotamatika hivi karibuni Mkoani hapa,kwa timu ya Damu Chafu kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa huo mara mbili mfurulizo.
Awari ya yote pongezi za kipekee ziwafikie waandaji wa michuano hiyo kituo cha Planet Redio chenye Makao yake Makuu Ghorofa la Mt Uluguru lililopo Mtaa wa Mlapakolo Kata ya Mji Mkuu .
Redio hiyo inayomilikiwa na Fred Mlingo ambaye baba yake mzazi ndiye Mlikiki wa Ghorofa hilo la hotel ya kisasa ya Mt Uluguru takribani miaka 4 mfurulizo ametoa kibali kwa vijana wake kuandaa mashindao hayo chini ya Nahodha wao Mkurugenzi wa vipindi Madam Warda Makongwa.
Ligi ya Msimu huu ilishirikisha timu 4 ambazo ni Wakushi Fc Kutoka kata ya Mafiga.Chaka Bovu Fc kutoka Kata ya Kiwanja cha Ndege,Black People’Taifa la Watu weusi’ kutoka Kata ya Mji Mpya na Mabigwa watetezi Damu Chafu Fc Kutoka kata ya Mwembesongo.
Timu hizo ziliingia moja kwa moja Nusu fainali ambapo Dmu Chafu walitinga fainali baada ya kuinyuka kwa mikwaju wa Penalti Black People huku Chaka Bovu walitinga fainali kwa njia hiyo hiyo ya Mikwaju ya Pelnati dhidi ya Wakushi Fc baada ya timu zote hizo kutoka sare dakika 90 za awari.
Kwenye mchezo wa Fainali uliohudhurika na mashabiki kibao waklongozwa na mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe Mussa Kilakala,Chaka Bovu walijaa kwenye mfumo wa Damu Chafu na kujikuta wakipokea kichapo cha bao 3-0 hali iliyopelekea kichaka chao kibovu kilichonyauka njasi kuunguzwa na Damu hiyo chafu.
Mara baada ya kutetea ubingwa huo walioutwaa Mwaka jana Damu Chafu walikabidhiwa zawadi wa Kombe na kitita cha Pesa Milioni 4 na Mgeni rasmi Mhe Kilakala.
Kufuatia timu hiyo kuweka rekodi ya mashindano hayo kutwaa kombe hilo mara mbili mfurulizo Mtandao huu ulitinga kwenye maskani ya Damu Chafu Mtaa wa Mafisa Kata ya Mwembesongo kwa lengo la kujua siri ya mafanikio ya timu hiyo kwenye mshindano hayo.
Baada ya kufika kwenye maskani ya timu hiyo iliyopo jirani na geti kuu la shule ya Msingi Mafisa A Mtandao huu ulirakiwa na Rais wa timu hiyo Ayub Aziz
Rais huyo alipotakiwa kueleza siri ya mafanikio hayo alisema ni umoja wa wachezaji, Viongozi na wananchi wa kata ya Mwembesongo,ambapo makundi yoye hayo yaliungana kwa hali na mali na kufanikisha jambo hilo.
“Siri kubwa ya sisi kutwaa kombe hili mara mbili mfurulizi ni kama ifuatavyo wachezaji na viongozi wa timu zote zilizopo kata ya Mwembesongo tumeweka kando tofauti zetu tumeungana kwa kushirikiana na wananchi wa kata hii kufanikisha jambo hilo.
Timu zilizopokata ya Mwembesongo ni Burnafaso Fc. Mangolo Fc. Assemble fc na Chadongo Fc”amesema Rais huyo na kuongeza.
“Kitu kingene ambacho wengi hawakijui namua kukuambia wewe shekidele ni kwamba ukuta mzima wa Damu Chafu wanalala na kuamka hapa Mafisa.
Mabeki hao ni Saddy Mapuya ambaye ni Nahondha .Said Mwande,Hamza Beta na Abuutwaribu Chachallo huyu ni kiungo mwingine ni mshambuliaji Jafaph Kipira”alisema Rais Ayub
Amesema wachezaji hao 5 ambao wapo kikosi cha kwanza mbali ya kuwa wachezaji kwa umuhimu wao wanaingia kwenye vikao vya viongozi ndio maana wanachezaji kwa kujitoa zaidi wakiwa na mapenzi ya dhati na timu yao ya Mtaani.
Alipoulizwa pesa hizo Milioni 4 wamezifanyia nini? Rais Ayub alijibu
”Kwa sababu swala hili lilikuwa la Kata tukisaidiwa na wananchi hivyo tumeamua kurejesha sehemu ya pesa hizo kwa kulipa Luku na bili za Maji kwenye misikiti 5 ya Kata ya Mwembesongo, kisha tumesoma dua ya kuwarehemu marehemu dua hiyo imekwenda sambamba na sadaka ya chakula, pesa zilizobaki tumewapa posho wachezaji na kulipa madeni”alimalizia kusema Raia huyo wa heshima.